
Lakini sasa anaweza akabadili mawazo na kwenda kujiunga na kocha ambaye alimtambulisha kwenye soka la kimataifa wakati akiwa na Barca.
Guardiola alisema: “Namataka Thiago Alcantara. Nimewaambia Bayern wafanye kila kitu kumsajili lakini sijui nini kitatokea.
“Thiago ni mchezaji pekee ninayemhitaji, hilo ndilo nililowaambia.
“Nimsajili yeye au nisisajili kabisa. Tuna wachezaji wengi lakini tunahitaji ubora wa ziada ambao Thiago Alcantara atauleta.
“Namfahamu Thiago vizuri sana. Nimeongea na mwenyekiti Rummenigge na mkurugenzi wa ufundi Sammer kuhusu kumsajili, sasa tusubiri tuone nini kitatokea.
“Sidhani kuongeza kiungo mwingine kutaleta tatizo kwetu. Nimeongea na klabu kuhusu mpango/wazo wangu na sababu za kumhitaji Thiago.
“Nimewapa mawazo yangu, ;alini naisikiliza bodi itasemaje. Wakikataa pia ni sawa.”
No comments:
Post a Comment